Tuesday, May 8, 2012

KESI YA ELIZABETH 

MICHAEL  LULU

 YASIKILIZWA

 LEO   

Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Kisutu jijini
 Dar es salaam. Bi
 Augustina Mmbando mapema leo msanii wa filamu 
Tanzania ambaye anahusishwa na kifo 
cha msanii mwenzake pia wa filamu Steven Kanumba
 amesimama kizimbani akikabiliwa na shtaka hilo
 huku mahakama ikiamuru mtuhumiwa huyo kutojibu lolote kuhusiana 
na kesi hiyo.Utata uliibuka wakati Mawakili wanao 
mtete Lulu Keneth Fungamtama, Fulgence Massawe, 
Peter Kibatala na Jackline De Meero, 
Ambapo Wakili  Fungamtama alidai Mahakamani hapo
 kwamba kutokana na umri mdogo wa mtuhumiwa wanaiomba
 Mahakama itoe udhuru kwa mtuhumiwa Elizabeth
 kushitakiwa katika Mahakama ya watoto kwa kuwa ana 
umri chini ya miaka 18 pia kesi yake iwe INCAMERA 
ombi ambalo lilitupiliwa mbali na mahakama hiyo 
kwa kutumia kifungu cha sheria namba 196  kuwa Mahakama hiyo
 haina mamlaka ya kusikiliza kesi za jinai hivyo ameahirisha  kesi hiyo 
 hadi Mei 21 mwaka huu  kesi hiyo itakapotajwa tena. 
Hivyo Lulu amerudishwa Segerea hadi kesi yake itakapotajwa tena. 

No comments:

Post a Comment